Popular Posts

Friday 27 November 2015

breaking newzzz: rais john pombe magufuli amemsimamisha kaz kamishna mkuu TRA!!!clik here ujionee

Aliyekuwa Kamishna wa TRA Rished Bade
Rais John Pombe Magufuli amemsimamisha kazi kamishna wa mamlaka ya mapato TRA Bw.Rished Bade na kumteua Bw.Philiph Mpango kukaimu nafasi hiyo.
Taarifa kutoka ikulu zimesema kuwa uamuzi huo wa rais Magufuli umefuatia ziara ya waziri mkuu bandarini uliobaini upotevu wa makontena 349.
Aidha rais Magufuli amemtaka Rished Bade kutoa ushirikiano kwa Philiph Mpango wakati uchunguzi ukiendelea.

Sunday 1 November 2015

breaking newzzz#!! kuwa ile nyumba anayo kaa super star diamond kumbe c yake!!!!? ....

nyumb anayoish ze super star platnumz!!!
inayo zaniw kuw c yake.n

amaxc blog: duh kumbe jina janeth n la aina yake..

first ladies weny jina hlo baran afrik

amaxc blog: le babyzz aliyetikisa mitandao dis wikiendi...

imekuwa kawaida sana kuwachek  mababyzz kwenye mitandao!!! such as insta, twitter na mingineyo miiingi
but huyu hapa ndo kauwa bendi wikiendi hii
unamjua n nani??????
stay tuned to amaxc..

amaxc blog: be ur own boss kwa kutumia nguvu kidogo tu!! kwa ufugaji kuku...

UFUGAJI WA KUKU WATANO (5) WA KIENYEJI UPATE KUKU MIA MBILI (200) KWA MIEZI SITA (6) TU! (Kuku 200 x 5,000 = 1,000,000) Unaweza ukaniona kama mimi ni kichaa na ninaye ota ndoto za mchana ambazo hazina mafanikio wala tija maana nadharia hii inaweza isiwaingie vizuri watu vichwani mwao. Watu wengi wamekuwa wakisema na kushauri hata kushauriwa hata na wale wasiofaa. Ninaamini wengi wetu hawapendi kuamini kile wanachoambiwa hadi pale watakapoona kwa macho yao ndipo waamini (akina Tomaso). Sikia nikuambie! kama huamini haraka kitu chochote hebu usimkatishe tamaa yule aliyekwambia habari hizo za kukatisha tamaa, badala yake jaribu kupeleleza na kufuatatilia hatua kwa hatua tena kwa makini maelezo uliyopewa, kisha yaweke katika utendaji (tenda/fanya) kwa ufanisi kisha subiri matokeo. Baada ya kupata matokeo sasa unaweza kwenda mbele kidogo ukauliza/ kusoma/kujifunza zaidi ili kuona kama kuna mahali umekosea au hukuzingatia kanuni na maelekezo uliyopewa. Baada ya kupata maelezo ya ziada hebu rudia kufanya tena kwa kuboresha kupitia maelekezo ya awali na hayo mapya uliyopata yote kwa pamoja ili upime matokeo yake. Hapo sasa utakuwa upo kwenye haki ya kuamini au kutoamini kwamba jambo hilo ni kweli au siyo kweli na siyo kutaa tu kwa ubishi usiokuwa na maana yeyote. Kwa kufanya hivi hakika utapiga hatua mbele katika kuboresha maisha yako ya sasa na ya baadae. Ila ukifanikiwa usije ukamkufuru Mungu aliyekuwezesha. Hebu anza na kuku Watano (5) tu Majike wenye Rika/Umri mmoja (au wanaokaribiana). Watunze vizuri kwa kuwapatia chakula kilicho na mchanganyiko kamili wa viini lishe vinavyotakiwa katika mwili wa kuku, yaani; wanga, protini, calcium, chumvichumvi, madini joto nk (kama nilivyoeleza hapa chini). Wawekee na Jogoo mmoja mzuri wa kienyeji/ kizungu/chotara (kama nilivyoeleza hapa chini juu ya uchaguzi wa majogoo). Wanapoanza kutaga watayarishie mahali pazuri/Kiota kizuri cha kutagia na kuatamia kwa kuwajengea viota ndani ya banda. Hakikisha mahali hapo hapavuji wala hapapati unyevunyevu wala joto kali sana. Hakikisha mahali hapo pana usalama wa kutosha (mahali wanyama hatari kama vicheche, pakashume, nyoka nk hawawezi kufika). Kuku wakiendelea kutaga na sasa ukaona wanakaribia kuatamia,Anza kuchagua aina ya mayai unayotaka kuku wako walalie. Hii inamaanisha kuwa; ukichagua mayai makubwamakubwa hayo yanakuwa na vifaranga majogoo na mayai madogomadogo mara nyingi huwa ni ya vifaranga majike. Acha kuwawekea mayai ya mviringo kama mpira! Hakikisha kuku wote wanasubiriana ili walalie/ waatamie kwa pamoja. Weka mayai 12 hadi 15 kwa kila kiota cha kuku 1 kulingana na umbo la kuku wako. Kuku anaweza kutaga hadi mayai 30 kwa kila msimu wa kutaga unapofika. Unaweza kutumia mayai machache kati ya 30 kwa kumuatamishia kuku wako huku mayai mengine yakisubiri awamu ya pili ya kuatamiwa.Kwa mfano ukiwawekea kuku wako hao watano, Kuku 5 x Mayai 12 = Mayai 60. Kwa kawaida kuku huatamia/hulalia mayai kwa siku 19 hadi 21/24 tu hadi anapototoa vifaranga. Hakikisha unawawekea kuku walioatamia chakula chenye viini lishe vya kutosha na maji mengi karibu na viota vyao ili wakitoka kwenye viota vyao wale chakula mara moja na kunywa maji kisha warudi haraka kwenye mayai yao. Hii itasaidia kuangua mayai yote 12/15 bila kuharibu yai hata moja. Au hata yakiharikbika basi hayataharibika mengi kama ukiacha kuwawekea chakula waende kufukuzana na panzi na vyakula majalalani huko nje na kuchelewa kurudi kwenye mayai yao. Wakati ukisubiria siku hizo 21/24 anza kujenga kibanda kidogo ndani ya banda kubwa ulilojenga awali au jikoni au andaa boksi kubwa na gumu kwaajili ya kutunzia vifaranga watakaoanguliwa ndani ya siku 21/24 zijazo. Baada ya kuku hao 5 kuangua vifaranga wako 60 hapo ndipo kazi kubwa ya kulea vifaranga inapoanza. Elewa kuwa ili upate mafanikio haraka hakikisha kuwa kazi ya kulea vifaranga inakuwa yako na siyo ya kuku! Kwanza, Unatakiwa kuondoa na kuchoma moto/kufukia mabaki yote ya mayai na kuboresha usafi wa banda lote ili kuepusha magonjwa kama vile kuharisha, viroboto, papasi nk. Hapo unaweza kuwatoa vifaranga wako wote 60 mmojammoja kadri wanavyoanguliwa hadi kufikia kifaranga wa mwisho, yaani Yule wa 60 na kuwaweka katika kibanda kidogo/boksi ulichokijenga na kuwawekea mayai mengine mama zao (yale 15/18 kati ya 30 uliyoyabakiza) ili waatamie tena kwa siku 21 hadi 24 zingine. Unapotoa kifaranga kutoka kwa kuku aliyeatamia humfanya kuku Yule ashindwe kutoka kwenye mayai maana hana mtoto wa kulea. Akimaliza kuangua mayai yote na ukamuwekea mengine ni rahisi kwake kuendelea kuatamia maana atasubiri kupata vifaranga na ndipo atajikuta amelalia kwa siku 21 zingine bila wasiwasi. Kwa kufanya hivyo utakuwa tayari umejipatia vifaranga/kuku zaidi ya 100 ndani ya wiki 7 tu! Sasa Unatakiwa kuwajali sana kuku hawa wanaolalia kwa mara ya pili kwa kuwapa chakula cha kutosha, maji, majani ya makongwe, mchicha, mchunga nk ili wapate vitamini na madini mengine muhimu kwa afya zao. Fanya hivyo hata watakapokuwa wametotoa na ukawanyang’anya vifaranga. Hii itawasaidia ili wasinyonyoke sana manyoya maana kuku wengi hunyonyoka manyoya wanapoatamia. Kwa kufanya hivi, kuku wako watakaa kwa wiki 2 hadi 3 bila vifaranga na kisha wataanza kutaga tena na kuatamia kama mwanzo. Vifaranga wako hakikisha unawatengenezea chumba chao kido ndani ya banda kubwa/ jikoni, kisha wawekee chanzo chochote cha joto kama vile; taa ya chemli/jiko la mkaa/ vizinga vya moto nk ili wasiathiriwe na baridi hasa wakati wa usiku. Umakini mkubwa sana unatakiwa hapa! Hakikisha unakuwa makini wakati wa usiku ili kuongeza na kupunguza joto ndani ya kibanda cha vifaranga maana wakati huu maranyingi joto hupungua na ubaridi huongezeka na hivyo unaweza kuua vifaranga wako. NAMNA YA KULEA VIFARANGA. Katika ulezi wa vifaranga kama kuku utawanyang’anya vifaranga vyao utatakiwa kuwajengea banda dogo (ndani ya banda kubwa/uzio) ili uwawekee chanzo cha joto kama taa/jiko la mkaa (kama ni sehemu/ majira ya baridi). Kama utatumia jiko la mkaa unatakiwa kuacha kwanza hadi mkaa mweusi uwake wote ndipo uweke bandani maana mkaa ukitoa moshi unaweza kuathiri vifaranga vyako. Angalia namna ya kuweka jiko lako la mkaa juu kidogo ili vifaranga wasiungue. Hakikisha taa yako haitoi moshi sana na haivujishi mafuta. Pia uwe na akiba ya mafuta ya taa ya kutosha. Usiweke mafuta mengi kwenye taa maana inaweza kulipuka ikakuletea hasara. Vifaranga wasizidi 50 kwa boksi 1. Hakikisha umewasha taa/jiko lako ndani ya boksi saa tatu au zaidi kabla ya kuwaweka vifaranga ili chumba/boksi lipate joto kabla ya vifaranga kuwasili. Njia hizi zinahitaji uangalifu wa hali ya juu sana kwani kuhatarisha/kuua vifaranga ni kuhatarisha maendeleo yako. Kama utaamua kutumia umeme pia ni vizuri zaidi maana inapunguza hatari zaidi. Kwa hiyoa njia zote tatu unaweza kutumia jedwali lifuatalo ili kuweza kumeneji joto la kibanda cha vifaranga; UMRI WA KKUKU/VIFARANGAJOTO NDANI YA BOX/KIBANDA CHA KULELEA VIFARANGAJOTO NDANI YA CHUMBA/BANDA Wiki 133-35oc30-32oc Wiki 230-33oc27-29oc Wiki 327-31c24-26oc Wiki 424-29oc21-23oc Wiki 526-27oc22-23oc Baada ya wiki ya 4/5 pasua box/watoe kwenye banda la kulelea ili walelewe kwa joto la kawaida la banda/chumba. Kwa kawaida joto hupimwa kwa kipimajoto (thermometer), lakini kama huna kipimo hiki, njia rahisi ni kuwaangalia kulingana na tabia zifuatazo; Kama vifaranga wamejikusanya sehemu moja basi joto ni kidogo bandani mwao, au kama wanaenda mbali na chanzo cha joto huku wanatanua mabawa yao na wakihema harakaharaka basi joto ni kali/ limezidi kiwango. Pale watakapo tawanyika vizuri ndani ya boksi/kibanda cha kulelea huku wanakula na kunywa maji vizuri basi joto ni la wasta na ndilo linalofaa. Kama unatumia njia ya Boksi, basi unatikiwa kulipanua kulingana na ukuaji na mahitaji ya vifaranga vyako. Vifaranga wako wape chakula cha vifaranga cha kutosha, maji safi na salama, majani mabichi ambayo hufungwa kwa kuning’inizwa kwa kamba,na CHANJO za minyoo nk ili wapate vitamin, madini na protini itakiwayo na kuzuia tabia ya kudonoana ili wakue vizuri. Hakikisha kuwa chumba chao ni kisafi na hakina unyevunyevu wakati wote. Unyevunyevu husababisha ugonjwa wa baridi na hufanya vifaranga wajikunyate na kutetemeka na wanaweza kufa ghafla! Inashauriwa kuwa siyo salama kufuga aina nyingine ya ndege kama vile njiwa, bata, bata mzinga nk kwa kuwachanganya na kuku maana kila aina ya ndege wanamagonjwa yao. Hivyo kuwachanganya kutakufanya ushindwe namna ya kuwatibu wanapopatwa na ugonjwa. Pia chawa wa njiwa huleta ugonjwa wa Ndui hasa kuku wanapoangua vifaranga wao. Hapa ugonjwa unaweza kufyeka vifaranga wako wote 60/100 kama utafuata ushauri wangu! Baada ya wiki 2 hadi 3 baada ya kuwanyang’anya vifaranga kuku wako wataanza tena kutaga mayai. Wakiatamia wote 5 Kama utaimarisha huduma kwao na kwa vifaranga/kuku wale 100 tayari utakuwa una kuku 105 au zaidi. Kuku wale 5 wa mwanzo wakiatamia tena kwa siku 21 hadi 48 (kama utafuata mfumo ule wa mwanzo wa kuaatamishia mara 2) utajipatia vifaranga wengine 100 tena na hivyo kuwa na kuku zaidi ya 200 ndani ya miezi 5/6 tu! Ukiwahudumia vifaranga wale wa mwanzo 100 vizuri kwa miezi 3 na nusu nao wataanza kutaga kama mama zao. kwahiyo, Chukulia walalie majike 5 wa mwanzo na majike 50 waliopatikana baada ya uzao wa kwanza kwa miezi ile 3 ya mwanzo utakuwa na mitetea 55. Wote wakiatamia na watoe vifaranga 10 kila mmoja kwa siku zilezile 21 hadi 46, tayari utakuwa na vifaranga 550! Sasa jumlisha na wale 150 waliobakia kati ya kuku 200 na wote wakakua vizuri utapata kuku na vifaranga zaidi ya 700! Jumlisha na 550 watakaototolewa na mama zao wale 5 wa kwanza na wale 50 wa uzao wa 1 na 2 kwa mara ya 2 si tayari utakuwa na kuku zaidi ya 1,200 ndani ya miezi 6 hadi 8 tu? Hivyo utajikuta unao kuku zaidi ya 1,000! Kati ya kuku 1,000 ukisema utoe kuku 800 wa kuuza na ukiwauza kwa bei ya Tsh. 4,000 kwa kila kuku 1 tayari utakuwa na Jumla ya Tsh. 3,200,000/= ambazo unaweza kufanya mtaji wa mambo mengine au kuboresha mradi wako zaidi. Unafikiri hapo hujaanza kufikia lengo la kuku 1 akuletee shilingi Milioni 1? Ukiendelea hivi inamaana kuku 1 atakuzalishia zaidi ya hapo. BANDA LA KUKU. Unatakiwa kuwa na banda bora la kufugia kuku ambalo litaweza kutunza kuku ili wasiweze kupatwa na madhara mbalimbali kama vile; kuliwa/kujeruhiwa na wanyama wakali, kuchukuliwa na wezi nk. Lakini banda bora pia litawasaidia kuku kuhimili mabadiliko mbalimbali ya hali ya hewa yanayoweza kujitokeza. Sehemu ambayo inafaa kwa ujenzi wa banda bora ni ile ambayo inaweza kufikika kwa urahisi, iwe na mwanga wa kutosha, isiwe na upepo mkali na isiyoruhusu maji kusimama au kuingia ndani. Banda ni vema likawa la ukuta/mbao/ mabanzi.matete/mianzi imara ili lishikilie paa vizuri lisianguke. Kuta hizi zaweza kujengwa kwa matofali ya saruji/matope/kuchomwa/ mabanzi/mbao nk. Katika kuezeka waweza kutumia mabati/vigae/nyasi. Banda ni vema likawa kubwa kulingana na kiasi cha kuku na umri walionao. Kitu cha kuzingatia ni kwamba banda liwe na hewa ya kutosha. Kuku wanaofugwa ndani ni vema wakatengenezewa uzio mpana (angalau Mita 8x10) ili wapate mahali wanapoweza kuota jua, kupumzikia/kupunga hewa na kufanya mazoezi (wawekee kamba/bembea/ngazi ndani ya banda). Hakikisha kuwa banda ni imara na hawatoki nje ya banda na kwenda mbali ili uweze kuwawekea chakula cha kutosha na maji na hata wale wanaotaga/kuatamia wapate chakula na kurudi haraka. Banda likiwa kubwa na bora litapunguza magonjwa kwani litakuwa na hewa ya kutosha ambayo itasaidia kupunguza joto na unyevunyevu usio wa lazima bandani mwako. Hii itasaidia uingizaji oksijeni ya kutosha na kupunguza hewa chafu zenye madhara kwa kuku. Pia litasaidia namna ya kufanya usafi kwa urahisi na kupunguza vumbi ambalo linaweza kusababisha kikohozi kwa kuku wako. Ni vema banda lisipungue Mita 3 kwenda juu. Mambo muhimu ndani ya Banda. Sakafu nzuri (iliyotengenezwa kwa saruji/ udongo ili isituamishe maji. Isiwe na nyufa ili iweze kusafishwa kwa urahisi. Hakikisha kuwa banda linakuwa na Viota (vitagio) vizuri kwaajili ya kutagia. Viota viwe na urefu wa Sentimita 30 na upana sentimita 30 na kina sentimita 35. Sehemu ya mbele izibwe kwa sentimita 10 tu chini. Sehemu zote hizo zizibwe kwa ubao. Kama kuku wako ni wakubwa unaweza kuongeza upana, urefu na kina kiasi cha kutosha mfano, Upana na Urefu 35cm, kina 55cm nk. Hakikisha kiota/kitagio kinakuwa na giza kiasi maana kuku hupenda kutaga mahala pa giza kidogo/palipojificha. Giza litasaidia kuku asiweze kula mayai au asiweze kudonoana na kuku wengine. Kiota pia kinatakiwa kiwe mahali ambapo ni rahisi kwa kuku kuingia na kutoka, pia iwe ni rahisi kusafisa. Ndani ya kiota kuwekwe majani makavu/ maranda ya mbao laini na kinyunyize dawa ya unga ya kuzuia viroboto/utitiri kabla ya kuweka nyasi. AIDHA, ni vizuri sana kuwawekea kuku wanaoatamia mayai wakati wa usiku maana ukimuwekea wakati wa mchana anaweza kuyaacha. Kuku anayetarajiwa kuatamia ni vema akachunguzwa kama anao utitiri/viroboto/ chawa kwenye manyoya yake. Wadudu hawa humkosesha raha kuku anayeatamia na wengi huacha mayai na kukimbia/wasitulie kwenye viota vyao. Hali inapelekea kuanguliwa kwa vifaranga wachache. Unaweza kumuona mtaalam wa mifugo kwa ushauri zaidi. Banda liwe na vichanja maana kuku hupenda kulala juu ya vichanja maana nao ni ndege. Vyombo safi na vizuri kwaajili ya chakula na maji. Walazie majani makavu/maranda ya mbao/ makapi ya mazao sakafuni kwa banda zima. UCHAGUZI NA UHIFADHI WA MAYAI. Mayai huharibika kwa urahisi sana yasipo tayarishwa na kutunzwa vizuri kwa uangalifu. Matayarisho huanzia bandani hadi ndani kwa kufanya yafuatayo; Hakikisha viota vyote ni safi wakati wote. Chakula kiwe ni cha kuimarisha gamba la yai na vyakula vingine. Vyombo vya kukusanyia mayai viewe safi na imara. Kusanya mayai mara2 hadi 3 kwa siku ili kuepuka mayai kuvunjwa/kuliwa/kuchafuka kwa mayai mengi na kupoa haraka. Ondoa mayai yaliyo na nyufa na maganda yasiyo imara. Safisha mayai mara baada ya kukusanya na kabla ya kuweka kwenye chombo cha kuhifadhia saa 12-24. Mayai yanaweza kuoshwa kwa maji ya uvuguvugu (nyuzijoto 35oc) na kusugua taratibu kwa mkono ili kuondoa uchafu (kama upo). Lakini unashauriwa kusugua kwa mkono bila maji ili kusafisha maana maji hupunguza ubora wa yai na maranyingi yai huharibika haraka. Weka katika vyombo visafi kwa kuelekeza sehemu ya yai iliyo pana iwe juu na sehemu nyembamba iwe chini, beba kwa uangalifu. Hifadhi mayai katika sehemu ya baridi nyuzijoto10 hadi 16 za sentigredi. Mayai yapangwe kwa daraja kwa kufuata ukubwa na rangi ili kuvutia wateja na kuongeza bei. Pia unaweza kuweka kwa kufuata muda unapoyaokota kutoka bandani. Weka lebo yenye tarehe ili usichanganye wakati wa kuwaatamishia kuku wako/kuuza. Kuchagua mayai ya kuatamishia kuku kwaajili ya kuangua vifaranga. Mayai yanayofaa kwa kuatamiwa na kuanguliwa ni vema yawe na ukubwa wa wastani, yasiwe na ufa/nyufa, yasiwe ya mviringo kama mpira, yasiwe na uchafu wowote juu ya gamba lake, yasiwe yametengwa kwa zaidi ya wiki 1 (siku 7). NJIA MBALIMBALI ZA UFUGAJI WA KUKU. Kuna njia kuu mbili za ufugaji wa kuku. Ufugaji Huria Aina hii ya ufugaji, kuku huachiwa huru wajitafutie chakula na maji wao wenyewe. Utaratibu huu hutumika zaidi kufugia kuku wa kienyeji ambapo mfugaji hupata hasara na pengine hupata faida kidogo maana kuku hukosa uangalizi na hawapewi chakula cha ziada. Faida. Haina gharama kubwa za ufugaji.

Wednesday 28 October 2015

amaxc blog: sentensi tano za mbowe akizungumza na waandishi wa habari trh 27 oktoba liveeee

Ni saa chache tu baada ya kuanza kutangazwa kwa matokeo ya Urais ya mwaka 2015 Tanzania ambapo leo October 27, 2015 mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kazungumza na waandishi wa habari. ‘Yako mambo mengi yanatendeka ya hujuma dhidi ya mgombea wetu LOWASSA ili asishinde kiti cha urais, sambamba na kujaribu kupunguza kwa nguvu isipokuwa halali idadi ya wabunge wa UKAWA kwa kutumia jeshi la polisi’- MBOWE ‘Leo ni siku ya tatu jeshi la polisi limewaweka ndani vijana wetu wa IT zaidi ya 100, huku wengine wakifikishwa mahakamani, Kwahiyo wao wenzetu wamejaribu kuvunja mfumo wetu wa mawasiliano, wametumia polisi kuharibu vifaa vyetu vya kuhesabia kura’ – Mbowe .l ‘Katika mifumo kama hiyo tunapata wakati mgumu sana kuamini kwamba tume inachokifanya pamoja na serikali yake kina nia njema kwa nchi yetu‘ – Mbowe

Friday 23 October 2015

amaxc blog: mbalon kwa kumtusi raisi jakaya na mwanae...

Mkazi wa mjini Moshi, Kyefa Joachim Makundi (33), leo amepandishwa kizimbani akikabiliwa na mashitaka ya kumtukana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete. Mbali na shitaka hilo, mshitakiwa huyo amesomewa shitaka lingine la kumtukana Ridhiwan Kikwete ambaye ni mtoto wa Rais Kikwete ambaye pia ni Mbunge wa Chalinze anayemaliza muda wake. Mshitakiwa huyo amefikishwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama ya mkoa Kilimanjaro, Joachim Tiganga na kusomewa mashitaka hayo na wakili wa Serikali Kanda ya Moshi, Agatha Pima. Wakili Pima amedai mahakamani kuwa Oktoba 17 mwaka huu katika baa ya Harambee iliyopo katikati ya mji wa Moshi, mshitakiwa alitumia lugha ya matusi dhidi ya Rais Kikwete na mwanae Ridhiwan. Ingawa matusi hayo hayakuandikwa kwenye hati ya mashitaka, lakini wakili Pima amedai kitendo hicho ni kinyume cha kifungu 89(1) (a) cha kanuni ya adhabu kama kilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002. Chini ya kifungu hicho, mtu yeyote anayetumia lugha ya matusi, kuudhi, au kudhalilisha dhidi ya mtu mwingine katika hali ambayo inaweza kusababisha uvunjifu wa amani anatenda kosa la jinai. Adhabu inayotolewa kwa mtu anayepatikana na hatia katika kosa hilo ni kifungo cha miezi sita jela. Hata hivyo, mshitakiwa amekana shitaka hilo ambapo mahakama imesema dhamana ilikuwa wazi ikiwa mshitakiwa atakuwa na wadhamini wawili watakaosaini hati ya dhamana ya Sh1.5 milioni kila mmoja. Source: Mwananchi

Saturday 17 October 2015

Friday 16 October 2015

amaxc blog: Ratiba ya mechi za Ligi Kuu Tanzania bara, Uingereza na Hispania October 17 na 18

<Michezo: Ratiba ya mechi za Ligi Kuu Tanzania bara, Uingereza na Hispania October 17 na 18 
 By team leader
 on October 16, 2015
 113 shares
... Baada ya mapumziko ya Ligi mbalimbali duniani ili kupisha mechi za kalenda ya FIFA kumalizika, weekend hii Ligi Kuu mbalimbali zinaendelea kwa michezo kadhaa kupigwa katika viwanja tofauti tofauti, huenda ukawa unataka kufahamu mechi za weekend hii zitakazochezwa za Ligi Kuu Tanzania Bara, Uingereza na Ligi Kuu Hispania hii ndio ratiba ya mechi za weekend hii. Ligi Kuu Tanzania bara mechi za October 17 na 18 vpl
Mechi zote za Ligi Kuu Tanzania bara zitachezwa saa 16:00 kwa saa za Afrika Mashariki Mechi za Ligi Kuu Uingereza weekend ya October 17 na 18
EPL
 Ratiba ya mechi za Ligi Kuu Uingereza kwa saa za Afrika Mashariki 
 Tottenham Vs Liverpool saa 14:45 Chelsea Vs Aston Villa saa 17:00 
 Crystal Palace Vs West Ham saa 17:00 Everton Vs Man United saa 17:00 Man City Vs Bournemouth saa 17:00 Southampton Vs Leicester City saa 17:00
 West Brom Vs Sunderland saa 17:00 Watford Vs Arsenal saa 19:30 
 Jumapili ya October 18
 Newcastle Vs Norwich saa 18:00
 Ratiba ya mechi za Ligi Kuu Hispania
LALIGA
 Ratiba za mechi za Hispania kwa saa za Afrika Mashariki
 Real Madrid Vs Levante saa 17:00 
 Eibar Vs Sevilla saa 19:15
 Barcelona Vs Rayo Vallecano saa 21:30 Valencia Vs Málaga saa 23:00
 Real Betis Vs Espanyol saa 23:05 
 Mechi za Jumapili ya October 18 Villarreal Vs Celta de Vigo saa 13:00
 Real Sociedad Vs Atl Madrid saa 17:00 Getafe Vs Las Palmas saa 19:15 Deportivo de La Coruña Vs Ath Bilbao saa 21:30

amaxc blog: Ndoa ina miaka 10, kumbe Nameless na Wahu waliwahi kuchokana? Kilichofuatia je?

Entertainment; Ndoa ina miaka 10, kumbe Nameless na Wahu waliwahi kuchokana? Kilichofuatia je? Ni raha kuwa na Familia, mtu na mke wake wote mnafanya kazi Industry moja halafu wote mnafanya poa na watu wanakubali kazi zenu.. hiyo ni raha sana kiukweli !! Pata picha Jay Z na Beyonce wake.. Lakini moja ya Familia ya mastaa walioteka soko la muziki East Africa, Nameless na Wahu ni mfano mzuri wa mastaa ambao wamedumu kwenye Ndoa yao kwa miaka 10 na wote wanafanya muziki… “Ndoa sio kitu rahisi, mnatakiwa kusomana na kila mmoja amkubali mwenzake vile alivyo… mnatakiwa kuheshimiana pia” >>> Hii ni nukuu ya alichokisema David Mathenge aka Nameless, staa wa muziki Kenya na mume wa Wahu. Wahu
Wahu na mmoja wa watoto wao. “Kuna wakati mimi na Wahu tunachokana, na najikuta nasema kwamba sikuhitaji tena na yeye anasema hivyo hivyo hataki kuniona tena…. Lakini mara nyingi tunaenda kwa washauri halafu mambo yanakuwa sawa… Tulianza uhusiano tukiwa wadogo sana wakati huo tuko Chuo… Tulipendana, tukakua pamoja.. Tumetafuta maisha pamoja na kwa sasa tuna msingi mzuri sana wa maisha yetu” >>> Nameless. Wako mastaa ambao wanaamini wakioa au kuolewa wanajiongezea majukumu na kufanya washuke kimuziki, unaweza kucheki mfano mzuri kwa hawa watu wetu wa +254, ndoa miaka 10 na wako pazuri tu !!

amaxc blog: Hii ndio Hospitali ya kwanza kufunguliwa kitengo cha kuhudumia Wanaume waliobakwa !!

Duniani: Hii ndio Hospitali ya kwanza kufunguliwa kitengo cha kuhudumia Wanaume waliobakwa !! Kesi za wanawake kubakwa au kudharirishwa kijinsia ni kitu ambacho kimesikika sana.. lakini ishu za matukio ya wanaume kubakwa sio stori ambazo zimesikika sana au kuzoeleka masikioni mwa wengi !!
Hii Hospitali imeangalia pia umuhimu wa kutoa huduma kwa wanaume ambao wamebakwa au kufanyiwa ukatili wa kijinsia, ni Hospitali ya Södersjukhuset ambayo iko Jiji la Stockholm, ndani ya Sweden. Uongozi wa Hospitali hiyo wameweka Kitengo cha Huduma ya Dharura kwa ajili ya kuhudumia Wanaume waliobakwa, Huduma kwenye Hospitali hiyo zinatolewa kwa saa 24 na kila siku kuanzia Jumatatu mpaka Jumapili…
Mmoja wa Viongozi wa Serikali alielezea umuhimu wa Huduma hiyo >>>>”Nadhani hii ni Kliniki ya kwanza Duniani, tumefanya Utafiti Mitandaoni na hatujaona kama kuna sehemu nyingine inatoa Huduma ya aina hiyo… Wanaume wote watahudumiwa bure kabisa… Ni matumaini yetu kwamba waathirika wengi wa matukio ya aina hiyo ambao huwa wanajificha, watajitokeza kuhudumiwa“ Huduma hii inaonekana kuwa na umuhimu wake kwa Wanaume wa Sweden, Takwimu zinaonesha kwa kipindi cha miaka minne kuanzia mwaka 2010 Sweden iliongoza kwenye Takwimu za matukio ya Wanaume kubakwa katika Nchi za Ulaya