Popular Posts

Friday 22 July 2016

CHID BENZ afunguka mazito kuhusu joh makini na ney wa mitego.......hatareeeee


Rapper Chidi Benz amefunguka kwa kusema kuwa hakuna msanii wa Hip Hop ambaye amefikia mafanikio yake huku akidai Joh Makini na Nay wa Mitego wametengenezwa ili waje kulishika game la muziki.

Akiongea na Uhuru FM Alhamisi hii, Chidi Benz amedai mpaka sasa hakuna msanii ambaye ameweza kufanikiwa na kufikia mafanikio ambayo aliyafikia katika kipindi cha nyuma.

“Sijamsikia yule mtu ambaye anafanya matukio kama mimi, yakuwa na msafara wa gari kumi, kusafiri kwenye show na watu 30, ukasikia watu 7 wamezimia kwenye show, bado sijawai kusikia matukio kama hayo labda bwana Joh Makini amefanya show Arusha wakazimia watu 9?,” alisema Chidi Benz.

“Lakini nawasikia hao, kama Joh Makini namsikia na namuona kwenye muziki huu the way wametengeneza yeye ndo awe ameshika hili game, lakini hana nguvu, sisemi hivyo kama namblock hapana, hata mashabiki wake ambao wananisikiliza wamwambie nakubali hapo alipo na watu wamekutengeneza wewe ukae pale na hauna nguvu yakusema mimi ni Joh Makini, najua ni msanii mzuri lakini mimi ni The King Kong,”

Aliongeza, “Kwa hiyo wapo wasanii wengi wametengenezwa, mfano Nay wa Mitego pia, ni kitu fulani kimetengenezwa. Shetta hafadhali toka ameanza kutoka alikuwa anatengenezwa ili afanye game yake,”

Rapper huyo kwa sasa anafanya poa na wimbo wake mpya ‘Chuma’ aliyomshirikisha msanii kutoka WCB, Raymond.
Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook

No comments:

Post a Comment