1. KUMSIKILIZA KILA MTU
Kama kila anayekuambia kitu kuhusiana na
unachofanya unamsikiliza nakuhakikishia hutopiga
hatua kubwa. Katika jambo lolote unalofanya kuna
watu watakutia moyo na kuna wengine
watakukatisha tamaa. Wapo watakaokwambia
haiwezekani au huwezi. Tena wanaokwambia
haiwezekani watakupa mpaka mifano ya
walioshindwa. Kama unataka kufikia mafanikio
makubwa acha kuwasikiliza watu wanaokukatisha
tamaa, chagua ni kitu gani unatafanya na anza
kukifanyia kazi mpaka ufikie mafanikio yako.
2. UNAFANYA KILE AMBACHO KILA MTU
ANAFANYA
Huwezi kuamini ila iko hivi, mafanikio makubwa
yanakuja pale ambapo unakwenda hatua ya ziada.
Kwenye kila unachofanya kuna hatua ya ziada
ambapo kama ukienda hatua hiyo utafikia
mafanikioa makubwa sana. Kama unaamka asubuhi,
unakwenda kazini, unafanya kazi ulizopangiwa, jioni
unarudi nyumbani, unalala na kesho unarudia tena
huo mzunguko sahau kuhusu mafanikio makubwa.
Kama unafanya biashara kama kila mtu
anavyofanya kwa mtindo huo huo na mbinu hizo
hizo ambazo kila mtu anayefanya biashara hiyo
anatumia unasogeza siku tu. Kama unataka kufikia
mafanikio makubwa NENDA HATUA YA ZIADA.
Kama unaishi maisha ya bwana mike utasubiri sana
na hutofikia mafanikio makubwa.
3. UNATUMIA MUDA HOVYO
Poteza milioni mia moja, unaweza kuzitengeneza
tena baada ya muda fulani, poteza sekunde moja
ndio umeisahau kabisa. Hakuna kitu chenye
thamani zaidi ya muda, lakini ndio tunautumia
kizembe kuliko kitu chochote kile. Ili uweze kufikia
mafanikio makubwa lazima uweze kuwa na
matumizi mazuri ya muda wako. Tunaishi kwenye
dunia yenye kelele nyingi, kuna vyombo vya habari,
simu, email, mitandao ya kijamii na maongezi
mengine yanayokusubiri wewe kila siku. Usipokuwa
makini unaweza kuona unakwenda na wakati
kumbe unakwenda nje ya mstari wa mafanikio.
kitabu kava tangazo
4. UNAPENDA MAJIBU YA HARAKA
Sijui ni kitu gani kimeharibu dunia kwa sasa ila
kizazi cha sasa kinapendelea majibu ya haraka
kuliko vizazi vivlivyopita. Unataka uanze biashara
leo na mwezi ujao uwe umetengeneza faida mara
mbili ya mtaji!! Yaani unataka upande mchungwa leo
na wiki ijayo uanze kula machungwa. Hakuna kitu
kama hicho ndugu yangu, mambo mazuri yanahitaji
subira na yanahitaji uvumilivu. Usidanganyike na
kelele unazopigiwa na watu kwamba fanya hivi
utafikia mafanikio ya haraka, hayo ni matangazo ili
kufaidisha biashara zao. Huwa napenda kutumia
mfano huu mara kwa mara, huwezi kuwachukua
wanawake tisa ukawabebesha ujauzito mmoja
ndani mwezi mmoja wakatoa mtoto, kama unatafuta
njia ya mkato ya kufikia mafanikio unaweza
kuyapata ila hutofika mbali.
5. UNA MATUMIZI MABOVU YA FEDHA ZAKO
Hili nalo linatabia ya kushangaza sana. Ukiangalia
kwa makini, waliofanikiwa kifedha wana matumizi
tofauti kabisa na wale wanaolalamika kutokuwa na
fedha kila siku. Wakati wale wenye fedha nyingi
wakitafuta sehemu za uwekezaji, wale wanaozipata
kidogo wanatafuta viwanja vya kuzitumbua. Hata
kama unapata fedha kidogo kiasi gani ni lazima uwe
na kiwango ambacho uaweka pembeni. Jilipe wewe
kwanza kwenye kila kipato unachopata na hii
itakusaidia kuweza kuwa na maisha yasiyo na hofu
juu ya fedha. Kujua zaidi jinsi ya kujilipa wewe
kwanza soma makala hii unamlipa kila mtu kasoro
huyu mmoja wa muhimu
HELLOW!!! WELCOME THIS IS AMAxc THE GLOBAL MEDIA AND NEWS SUPPLIERS!!! amaxc.blogspot.com
Popular Posts
-
Duh hii ni aibu kwelikweli kuona msomi ambaye anategemewa kama kiongozi wa kesho kufanya mambo ya ajabu namna hii .. haya ni ...
-
Hii ni picha ya moja kati ya wanachuo msichana akiwa hosteli na ..demu huyo sio siri anawachanganya wengi chuo hapo ikiwemo ma lectur....
-
Mrembo mwenye ushawishi mkubwa zaidi kwenye social media hapa Bongo, ambaye alishawahi kujinyakulia taji kubwa zaidi la ulimbwende hapa Bon...
-
Ikiwa leo ndio Uchaguzi wabunge wa Viti Maalum Kupitia Chama cha Mapinduzi Nchini katika Mkoa wa Singida Mgombea Wema Sepe...
-
Hz n baadh ya pcha za shilole akiwa na boy wake!! wakiwa kweny mapoz ya mahab ***** { clik here to see the video wakiwa wanaoga ...
-
john pombe magufuli Edward Ngoyai Lowassa. Uchunguzi uliofanywa na Timu ya Uwazi Mizengwe hivi karibuni na kuihusisha mikoa yote ya Ta...
-
Mwanamke aliye bambwa na sungusungu akifanya mapenzi kwenye kichaka na dereva wa teksi.Richard Bukos na Issa Mnally Mwanam...
-
Hzi n baadhi ya pcha za mastaa tofauti w KIKE hapa tz . sio siri n balaa coz sometmes najiuliza ! do they ril care???? ? ...
-
Kutoka kutangaza kutafuta mume Instagram hadi kukiri kumpenda Uhuru Kenyatta, Ray C anaendelea kutengeneza vichwa vya habari Afrika Masharik...
-
Blogu ya Wananchi Wednesday, August 19, 2015 TUJIKUMBUSHE HABARI KAMILI YA KAMATI TEULE YA BUNGE YA RICHMOND TAARIFA HII HAPA LIVE YA MWAKA ...
Thursday 30 July 2015
AMAxc BLOG: KAMA UNATABIA HIZI HUWEZI KUFANIKIWA KWENYE MAISHA YAKO!!!!!
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment