*** Mtu mmoja amefariki dunia na mwingine kujeruhiwa wakati watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi waliposimamisha daladala eneo la Jangwani na kuingia ndani kupora mkoba unaosadikiwa kuwa na fedha.
Watu hao, waliokuwa na pikipiki aina ya boxer, walikuwa wakifuatilia basi hilo linalofanya safari zake kati ya Kariakoo na Mwenge na kulisimamisha eneo la Jangwani saa 7.30 mchana na baadaye kuwaamuru abiria wote wainame kabla ya kuelekea kiti cha nyuma alikokuwa amekaa mtu huyo aliyekuwa amebeba mkoba.
Mmoja wa abiria wa daladala hilo, Rehema Michael alisema wakati basi lao likiwa linaenda taratibu, alimuona mtu aliyekuwa amepakizwa kwenye pikipiki akishuka na kumfuata dereva na kisha kumuelekezea bastola usoni, akimtaka asimamishe gari.
Alisema dereva wao alitaka kukunja kona kuelekea Jangwani, lakini akatii amri na ndipo dereva wa bodaboda alipokwenda nyuma ya daladala na kumtaka mmoja wa abiria aliyekuwa amekaa nyuma ya daladala kutoa begi, huku mwingine akipiga risasi hewani, lakini hakupewa mkoba huo.
“Baada ya kuona yule abiria anakaidi agizo lao, mmoja wa majambazi hao alimpiga risasi ya kichwani na kifuani na kuanguka chini huku yule abiria mwenzake ambaye alipewa begi hilo alishike alilitupa chini na mmoja wa majambazi aliingia ndani ya daladala na kulichukua,” Hashim Ally.
Shuhuda mwingine, Richard Urio alisema wakati uvamizi huo ukitokea abiria walikuwepo ndani ya daladala hiyo akiwemo konda walilazimika kulala chini baada ya kusikia milio ya risasi zilizokuwa zikipigwa hewani, na kwamba baada ya kuchukua lile begi walimpiga risasi abiria mwingine ambaye alikuwa karibu na marehemu baada kuhisi alikuwa akizuia begi lisitolewe.
“Siti ya nyuma walikuwa wamekaa abiria wanne, na wawili kati yao walikuwa wamasai ambao mmoja wapo alikuwa amevaa begi mgongoni ambalo lilichukuliwa na majambazi baada ya kumuua mmoja wa wamasai huku mwingine akijeruhiwa na bastola shavuni,”Urio.
Shuhuda mwingine, Regina Mateso alisema yeye alipanda daladala hiyo eneo la Shakilango na kuwakuta wamasai hao ambao inasemakana walikuwa na fedha nyingi kutokana na maongezi yao.
“Wale wamasai walikuwa wanapigiana mahesabu na wapi kwa kwenda kubadilisha fedha. Yule aliyefariki alikuwa anamwambia mwenzake ukibadilisha hizi dola unapata Sh16 milioni, hivyo inawezekana wale abiria walikuwa na kiasi hicho cha fedha ambacho walikuwa wameweka katika begi la mgongoni,” Mateso.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Polisi Ilala, Lucas Mkondya alisema tukio hilo limetokea na wanalifanyia kazi .
“Na sisi polisi tumelipata sasa hivi ndio kwanza tunalifanyia kazi likikamilika tutatia taarifa,” Mkonya
HELLOW!!! WELCOME THIS IS AMAxc THE GLOBAL MEDIA AND NEWS SUPPLIERS!!! amaxc.blogspot.com
Popular Posts
-
Duh hii ni aibu kwelikweli kuona msomi ambaye anategemewa kama kiongozi wa kesho kufanya mambo ya ajabu namna hii .. haya ni ...
-
Hii ni picha ya moja kati ya wanachuo msichana akiwa hosteli na ..demu huyo sio siri anawachanganya wengi chuo hapo ikiwemo ma lectur....
-
Mrembo mwenye ushawishi mkubwa zaidi kwenye social media hapa Bongo, ambaye alishawahi kujinyakulia taji kubwa zaidi la ulimbwende hapa Bon...
-
Ikiwa leo ndio Uchaguzi wabunge wa Viti Maalum Kupitia Chama cha Mapinduzi Nchini katika Mkoa wa Singida Mgombea Wema Sepe...
-
Hz n baadh ya pcha za shilole akiwa na boy wake!! wakiwa kweny mapoz ya mahab ***** { clik here to see the video wakiwa wanaoga ...
-
john pombe magufuli Edward Ngoyai Lowassa. Uchunguzi uliofanywa na Timu ya Uwazi Mizengwe hivi karibuni na kuihusisha mikoa yote ya Ta...
-
Mwanamke aliye bambwa na sungusungu akifanya mapenzi kwenye kichaka na dereva wa teksi.Richard Bukos na Issa Mnally Mwanam...
-
Hzi n baadhi ya pcha za mastaa tofauti w KIKE hapa tz . sio siri n balaa coz sometmes najiuliza ! do they ril care???? ? ...
-
Kutoka kutangaza kutafuta mume Instagram hadi kukiri kumpenda Uhuru Kenyatta, Ray C anaendelea kutengeneza vichwa vya habari Afrika Masharik...
-
Blogu ya Wananchi Wednesday, August 19, 2015 TUJIKUMBUSHE HABARI KAMILI YA KAMATI TEULE YA BUNGE YA RICHMOND TAARIFA HII HAPA LIVE YA MWAKA ...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment